Psalms 9:1-6
Shukrani Kwa Mungu Kwa Ajili Ya Haki Yake
(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Muth-Labeni. ▼▼ Muth-Labeni ni mtajo mmojawapo katika lugha za muziki. Zaburi Ya Daudi)
1 ▼
▼ Zaburi hii ikiunganishwa na ya 10 zimetungwa kila beti likianzia na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22.
cEe Bwana, nitakutukuza kwa moyo wangu wote,nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu.
2 dNitafurahi na kushangilia ndani yako.
Nitaliimbia sifa jina lako, Ewe Uliye Juu Sana.
3 Adui zangu wamerudi nyuma,
wamejikwaa na kuangamia mbele zako.
4 eKwa maana umetetea haki yangu na msimamo wangu;
umeketi kwenye kiti chako cha enzi,
ukihukumu kwa haki.
5 fUmekemea mataifa na kuwaangamiza waovu;
umeyafuta majina yao milele na milele.
6 gUharibifu usiokoma umempata adui,
umeing’oa miji yao;
hata kumbukumbu lao limetoweka.
Copyright information for
SwhKC