Psalms 9:1-6

Shukrani Kwa Mungu Kwa Ajili Ya Haki Yake

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Muth-Labeni.
Muth-Labeni ni mtajo mmojawapo katika lugha za muziki.
Zaburi Ya Daudi)


1
Zaburi hii ikiunganishwa na ya 10 zimetungwa kila beti likianzia na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22.
cEe Bwana, nitakutukuza kwa moyo wangu wote,
nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu.

2 dNitafurahi na kushangilia ndani yako.
Nitaliimbia sifa jina lako, Ewe Uliye Juu Sana.


3 Adui zangu wamerudi nyuma,
wamejikwaa na kuangamia mbele zako.

4 eKwa maana umetetea haki yangu na msimamo wangu;
umeketi kwenye kiti chako cha enzi,
ukihukumu kwa haki.

5 fUmekemea mataifa na kuwaangamiza waovu;
umeyafuta majina yao milele na milele.

6 gUharibifu usiokoma umempata adui,
umeing’oa miji yao;
hata kumbukumbu lao limetoweka.

Copyright information for SwhKC